WANASIASA nchini wamedaiwa kuingilia shughuli za benki za
vijijini (vikoba), hivyo kuwafanya wananchi kushindwa kujikwamua katika
hali ngumu ya umaskini.
Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa waratibu wa mkoa wa vikoba, Edward Mlowe, katika mkutano wa taifa wa robo mwaka uliofanyika ukumbi wa Princes, Sinza, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka mikoa mbalimbali.
Mlowe alisema kikwazo hicho kwa wanasiasa kinakuja pale wanapoitisha mikutano ya kutaka kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na vikundi hivyo lakini cha kushangaza wanawahadaa kutoshiriki kwa kuhofia kwamba huenda kuna mpinzani mwenzao katumia vikoba kuwarubuni wananchi wake.
Hata hivyo mratibu huyo alisema maeneo ambayo yamekuwa yakitokea matukio kama hayo ni kwa wakuu wa mikoa ambao wamekuwa wakiwapa ushirikiano wa kutosha.
Mwenyekitii wa Vikoba taifa, Teddy Sanga, alitaja changamoto nyingine wanazokabiliana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kuwa ni pamoja na ukosefu wa elimu na mitaji kwa wanachama.
Ili kukabiliana na hali hiyo alisema vikoba imekuwa ikitoa elimu ya ujasiriamali kwa wanachama hao ili kusaidia kuwabadilisha kifikra na kimtazamo na kujitambua kwamba kwa kiasi kidogo cha fedha walichonacho wanaweza kuanzisha hata biashara ndogondogo ambazo baadaye zinakuja kuwa kubwa.
Diwani wa Kata ya Yakobi, mkoani Mbeya (CCM), Ester Mgeni, alisema Vikoba katika Mkoa wao imewasaidia wananchi wengi kuondokana na umaskini.
“Wanasiasa wenzangu wanapaswa kuelewa kwamba huwezi kumuongoza mtu ambaye ni maskini, hivyo vikoba ni moja ya eneo maalumu ambalo litawawezesha wananchi wetu kuondoka huko walipo na kuwa watu ambao wataweza kujiendeleza kimaisha,” alisema Mgeni.
Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa waratibu wa mkoa wa vikoba, Edward Mlowe, katika mkutano wa taifa wa robo mwaka uliofanyika ukumbi wa Princes, Sinza, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka mikoa mbalimbali.
Mlowe alisema kikwazo hicho kwa wanasiasa kinakuja pale wanapoitisha mikutano ya kutaka kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na vikundi hivyo lakini cha kushangaza wanawahadaa kutoshiriki kwa kuhofia kwamba huenda kuna mpinzani mwenzao katumia vikoba kuwarubuni wananchi wake.
Hata hivyo mratibu huyo alisema maeneo ambayo yamekuwa yakitokea matukio kama hayo ni kwa wakuu wa mikoa ambao wamekuwa wakiwapa ushirikiano wa kutosha.
Mwenyekitii wa Vikoba taifa, Teddy Sanga, alitaja changamoto nyingine wanazokabiliana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kuwa ni pamoja na ukosefu wa elimu na mitaji kwa wanachama.
Ili kukabiliana na hali hiyo alisema vikoba imekuwa ikitoa elimu ya ujasiriamali kwa wanachama hao ili kusaidia kuwabadilisha kifikra na kimtazamo na kujitambua kwamba kwa kiasi kidogo cha fedha walichonacho wanaweza kuanzisha hata biashara ndogondogo ambazo baadaye zinakuja kuwa kubwa.
Diwani wa Kata ya Yakobi, mkoani Mbeya (CCM), Ester Mgeni, alisema Vikoba katika Mkoa wao imewasaidia wananchi wengi kuondokana na umaskini.
“Wanasiasa wenzangu wanapaswa kuelewa kwamba huwezi kumuongoza mtu ambaye ni maskini, hivyo vikoba ni moja ya eneo maalumu ambalo litawawezesha wananchi wetu kuondoka huko walipo na kuwa watu ambao wataweza kujiendeleza kimaisha,” alisema Mgeni.
No comments:
Post a Comment